Jumatatu, 5 Machi 2018

FAHAMU KUHUSU SEHEMU YA MTANDAO WA INTANETI ILIYOFICHWA (DEEP WEB NA DARK WEB)

Hakika ulimwengu huu una mambo mengi ambayo hatuyafahamu bado, kila siku tunaweza kujifunza jambo jipya hadi mwisho wa maisha yetu.
Intaneti ni kitu ambacho kwa ulimwengu huu wa sasa kila mtu anakitumia kwa njia moja au nyingine. Jambo la kushangaza ni kuwa pamoja na kutumika huku kwa intaneti bado kuna mambo mengi ya kushangaza tusiyoyajua.
Je wajua kuwa ipo sehemu ya mtandao wa intaneti iliyofichwa? Sehemu hii inajulikana kama Deep web na Dark web.
Karibu ufuatilie makala hii ili nikufahamishe juu ya sehemu hii ya mtandao wa intaneti iliyofichwa (Deep web na Dark web)
Deep web ni nini?
Deep web ni sehemu ya intaneti ambayo haionekani kwenye injini pekuzi kama vile Google na Bing — moja kwa moja injini pekuzi haziwezi kuona sehemu hii kwa sababu imefichwa isionekane.
Deep web siyo kitu kilicho nje ya huu ulimwengu bali ni kitu ambacho umekuwa ukikitumia mara kwa mara — barua pepe yako, benki mtandao, meseji zako za Twitter, LinkedIn n.k Taarifa hizi haziwezi kuonekana kwenye injini pekuzi kwa kuwa zinalindwa kwa nywila (password) au kulipiwa ili kuziona.

“Vitu vyote visivyoweza kupatikana kwenye uso wa juu wa mtandao kwa kutumia injini pekuzi ni sehemu ya Deep web”
Ikizingatiwa kuwa tuna mabilioni ya watumiaji wa mtando wa intaneti duniani, hivyo inaelezwa kuwa kuna mamilioni ya taarifa au data zilizoko kwenye Deep web.

Hata hivyo inaminika kuwa Deep web inaunda sehemu kubwa ya mtandao; Deep web inaweza kuonwa kwa kutumia kivinjari (browser) cha kawaida kama vile Chrome na Firefox.

Dark web ni nini?

Dark web siyo sehemu tofauti na intaneti bali ni sehemu ya Deep web ambayo haiwezi kuonwa kwa kutumia kivinjari (browser) cha kawaida.

Kwa nini Dark web haiwezi kuonwa kwa kivinjari cha kawaida? Ikizingatiwa kuwa shughuli nyingi zinazofanyika kwenye Dark web ni haramu, si rahisi wahusika wake kuruhusu mambo haya kuonekana kwenye vivinjari vya kawaida.

Je kwenye Dark web kuna shughuli gani?

Uuzaji wa madawa ya kulevya
Uhalifu wa kila namna (uuzaji wa viungo vya binadamu, ajira za kutisha, ugaidi n.k)
Wadukuzi hatari wa kompyuta
Uuzaji wa taarifa na vitu vilivyoibiwa
Picha za unyanyasaji wa kingono hasa watoto
Uuzaji wa silaha
Mawasiliano ya wanaharakati na waandishi wa habari wanaotaka kuibua maswala mbalimbali. Hutumia njia hii kujificha wasije wakakamatwa na serikali au mahasimu wao. Mtandao wa wikileaks unapokea pia taarifa kupitia Dark web.
Je tovuti za Dark web zinaperuziwaje?

Tovuti za Dark web zinaishia na anwani mtandao (domain) zenye .onion, ambazo zinaweza kufunguliwa kwa kutumia kivinjari cha Tor pekee.

Tor ni kivinjari (browser) cha namna gani?

Tor ni kivinjari kilichotengenezwa na watu wakujitolea (voluntiers) kutoka sehemu mbalimbali duniani, ambacho hufanya kazi kwa usiri wa hali ya juu wa kuficha mawasiliano pamoja na watumiaji wake.

Hivyo mtu anayetembelea tovuti fulani au kufanya chochote kwenye mtandao kwa kutumia kivinjari hiki siyo rahisi kubainika.

Kwa mfano unaweza ukawa unaperuzi mtandao kwa kutumia Tor ukiwa Tanzania lakini ukaonekana mara uko Japan, mara Uingereza au hata Marekani.T browser

Ikumbukwe kuwa kutembelea Dark web siyo kinyume cha sheria lakini kufanya vitu huko kunaweza kuwa kinyume cha sheria kutokana na tovuti nyingi kufanya vitu vinavyokiuka sheria.

Kwenye Dark web siyo mahali panapovutia kama sehemu ya kawaida ya mtandao wa intaneti tulio uzoea. Tovuti nyingi huku zimetengenezwa kwa makusudi maalumu au pengine ya siri, hivyo hazikujali wala kukulinda.

Ili kuperuzi kwenye Dark web ni lazima uwe na kiungo (link) cha tovuti unayotaka kutembelea kinachoishia na .onion kwa mfano http://zqktlwi4fecvo6ri..onion (ukitaka kuifungua ondoa nukta moja) Hii ndiyo Dark web, hakuna kugoogle hapa; mambo yanaenda kwa namna ya ajabu ajabu tu.

Je Dark web ni mbaya?

Hapa kuna majibu mawili ndiyo na hapana. Pamoja na kuwa shughuli nyingi zinazofanyika kwenye Dark web sio halali, bado kuna toleo lake la Facebook na ProPublica kwa anauani ya .onion.

Lakini ukumbuke kuwa wachambuzi wa mambo wanasema tovuti hizi zinaweza zisiwe za kweli, kwani si rahisi Fecebook kukubali watumiaji wake kutumia anwani za kujificha za .onion. Hivyo kuwa makini na taarifa zako za siri huku.

Uzuri wa Dark web ni kuwa inawawezesha waandishi wa habari, wanaharakati na wale wanaoibua taarifa za siri kuwasiliana na kubadilishana taarifa bila wao kujulikana.

Ni wazi kuwa hakuna kitu kibaya kwenye mtandao bali ni matumizi pekee ndiyo hukifanya kiwe kibaya.

Neno la mwisho

Naamini umejifunza mengi ambayo hukuwa unayafahamu kuhusu sehemu ya intaneti iliyofichwa. Lakini pamoja na hayo uliyojifunza ningependa kukushauri kuwa makini sana kama utaamua kutumia Dark web. Kumbuka pia kuzingatia sheria kwani uhalifu, maovu na ukatili wa kutisha umejaa kwenye Dark web.

Kwa mfano picha za video za watu wakichinjwa, ubakaji wa watoto, wizi, chuki na ubaguzi husambazwa bila woga wowote. Wadukuzi hatari pia wamejaa kwenye Dark web, hivyo epuka kutoa taarifa zako, kupakua kitu chochote au kufanya muamala wowote.

Didas Tumaini

Jumamosi, 3 Machi 2018

USHAHIDI: "VICARIUS FILII DEI" NI 666.
_
Wakatoliki wamekuwa wakipinga mara nyingi kwamba Vicarius Filii Dei sio jina la papa na wala haina hesabu ya 666. Ukurasa mmoja wa Facebook wa majeshuiti unaoitwa "Asali Itokayo Mwambani" umejaribu kupotosha watu kwamba Vicarius Filii Dei kamwe sio jina la papa, na haifiki 666 kwa kuwa "u" haiwezi kugeuzwa na kuwa "v"! Hii hapa ni njia nyepesi ya kufunua uongo huu wa kijeshuiti. Tutazingatia Mambo mawili yafuatayo.
,
MOJA: Je "u" haiwezi kuwa "v" katika kilatini?
,
?Hii ni njia moja ambayo hawa majeshuiti wa katoliki wanaitumia kusema kuwa Vicarius Filii Dei haiwezi kuwa 666 kwa kuwa "u" huwezi kuigeuza na kuwa "v"! SASA nadhani kwa muda huu ungewapa hawa majeshuiti "A" au hata ungewapa "100%" kwamba wako sawa! Lakini kabla hujawapa hiyo "A", tafadhari tafuta dokomenti au sarafu za mapapa kisha uone herufi "u" ambavyo katika kilatini imeandikwa kama "v"; nitakusaidia kwa kukupa mifano halisi michache ifuatayo ambayo itaziba kabisa midomo yao.
,
a. Jina la papa "Pius" XI, limeandikwa kama "Pivs" kwenye medari yake ya mwaka 1929 iliyotolewa kwa ajili ya mkatabwa wa Lateran (angalia picha:  https://sabbathlight.files.wordpress.com/2017/11/1929.jpg).
,
b. Jina la papa "Paulus" VII, limeandikwa kama "Pavlvs" kwenye sarafu 100 Lire ya Vaticano ya mwaka 1963 (angalia picha: (https://sabbathlight.files.wordpress.com/2017/11/1963.jpg).
,
Hivyo utaona wazi jinsi gani Wakatoliki wanajifunua wenyewe kwamba "u" pia ni "v". Na kama ukichukua "Vicarius Filii Dei" na kuigeuza kuwa "Vicarivs Filii Dei" utapata 666:
V. . . . . .5
I. . . . . . 1
C. . . . . .100
A. . . . . .0
R. . . . . .0
I. . . . . . .1
V. . . . . . 5
S. . . . . . 0
= . . . . . 112
_
F. . . . . . .0
I. . . . . . . 1
L. . . . . . .50
I. . . . . . . .1
I. . . . . . . .1
=. . . . . . .53
_
D. . . . . .500
E. . . . . . . 0
I. . . . . . . .1
=. . . . . . 501
_
VICARIVS = 112
FILII        =   53
DEI          =  501
Jumla      =  666.
#  #  #  #  #  #  #  #  #  #  #  #  #  #
MBILI: Je VICARIVS FILII DEI sio jina la papa?
,
HUU ni uongo mwingine ambao wakatoliki huutumia kukataa namba 666 kwamba haimhusu papa. Wanasema papa kamwe hajawahi kutumia, na wala hata sasa hatumii jina hilo la Vicarivs Filii Dei. Hii ni njia nyingine ambayo makuhani na viongozi wa katoliki huitumia kuwaliwaza makundi yao ili kamwe wasije kuona ukweli. VICARIVS FILII DEI ni jina la papa na kuna maelfu ya ushahidi wa jina hilo kutoka kwa dokomenti za wakatoliki wenyewe. Hapo chini tutaangalia dokomenti chache katika hizo. (Msisitizo wa kwangu).
_
Gazeti la katoliki la "Our Sunday Vistors" katika mwaka 1914 liliandika kwamba:
,
“Jina la Papa katika Roma ni Vicarius Filii Dei. Jina hili limeandikwa kwenye kilemba chake[*]; na kama ukizichukua herufi za jina lake ambazo zinawakisha namba za Kilatini na kuzijumlisha kwa pamoja zinaleta 666.” —(Our Sunday Visitor, (Gazeti la Katoliki la kila wiki), November 15, 1914, chini ya ‘Bureau of Information’, p. 3)). [angalia nakala ya gazeti hili hapa: http://remnantofgod.org/osv1914.htm)
,
Mwaka uliofuata, ambao ni mwaka 1915 gazeti lilelile la Our Sunday Vistor likaandika tena kwamba:
,
"Maneno yaliyoandikwa katika kilemba cha Papa ni haya VICARIUS FILII DEI ambayo ni ya kilatini kwa ajili ya ‘KASISI WA MWANA WA MUNGU’. Wakatoliki huchukulia kwamba kanisa ambalo ni jumuiya ya kuonekana, lazima liwe na kichwa cha kuonekana. . . Maadui wa Upapa hukanusha jina hili kama dhana mbaya lakini Biblia inatuambia kwamba Kristo hakuwapa Kanisa lake mamlaka ya kufundisha tu, bali pia mamlaka ya kutawala. Kudai kuwa na mamlaka ya kutawala katika ufalme wa Kristo wa kiroho, katika nafasi ya Kristo , sio madhara zaidi kuliko kudai kuwa na mamlaka ya kufundisha kwa jina la Kristo.” —(Our Sunday Visitor, (Gazeti la Katoliki la kila wiki), April 18, 1915, swali la 30 chini ya ‘Bureau of Information’, p. 3)). [angalia nakala ya gazeti hili hapa: http://remnantofgod.org/osv1915.htm]
,
Tangu ukweli wa 666 ujulikane, mapapa walisimama kulitumia jina la Vicarius Filii Dei kwa wazi, ili kuwadanganya wakatoliki kwamba sio jina la papa, lakini dokomenti zao zenyewe zinawafunua. Kadinali Manning anasema:
,
"Ilikuwa ni utii wa heshima kusujududu kwa KASISI WA MWANA WA MUNGU, na kusuluhisha usuluhisho wa malalamiko yao kwa mtu ambaye wote wangekubali kutii.” —(The Temporal Power of the Vicar of Jesus Christ, pp. 231-232 na Henry Edward Kadinali Manning, toleo la pili, London: Burns and Lambert, 1862).
,
Kasisi wa Mwana wa Mungu = Vicarius Filii Dei.
,
Angalia Dokomenti za kilatini zifuatazo kutoka kanisa katoliki, ambazo kwa wazi zinatumia jina Vicarius Filii Dei. Moja inatoka kwenye kitabu kinachoitwa "Prompta Bibliotheca" kilichoandikwa na Lucius Ferraris; ambacho Insaiklopedia ya Ukatoliki inasema kimejaa maelezo ya thamani:
,
“Ut sicut Beatus Petrus in terris VICARIUS FILII DEI fuit constitutus, ita et Pontifices eius successores in terris principatus potestatem amplius, quam terrenae imperialis nostrae seremitatis mansuetudo habere videtur.” —(Prompta Bibliotheca Canonica, Juridica, Moralis, Theologica, Ascetica, Polemica, Rubristica, Historica, by Lucius Ferraris, Volume V, makala ya “Papa, Article II”, yenye kichwa “Concerning the extent of Papal dignity, authority, or dominion and infallibility”, point #20, column 1828, ilichapishwa katika Petit-Montrouge (Paris) na J. P. Migne, toleo la 1858)). [angalia dokomenti yenyewe hapa: http://www.lightministries.com/id788.htm]
,
Ikitafsiriwa kwa kiswahili dokomenti hii inasomeka: “Kama vile Petro mbarikiwa alivyofanyika KASISI WA MWANA WA MUNGU duniani, kwa hiyo inaonekana kwamba maaskofu wakuu, waandamizi wake, wanashikilia kutoka kwetu na ufalme wetu nguvu ya ukuu duniani ya juu kuliko uzuri wa utulivu wetu wa kifalme duniani.”
,
Dokomenti nyingine ya kilatini inayotumia jina hilo inasema:
,
“Beatus Petrus in terris VICARIUS FILII DEI videtur esse constitutus.” —(Decretum Gratiani, prima pars, dist. xcvi, col. 472, (kwanza ilichapishwa katika Bologna mwaka 1148, na ikachapwa tena mwaka 1555)). Dokomenti hii ilitafsiriwa katika kiingereza na Christopher B. Coleman, Ph. D., katika kitabu kinachoitwa “The Treatise of Lorenzo Vallo on the Donation of Constantine,” p. 13. New Haven: Yale University Press, 1922.
,
Ikitafsiriwa katika kiswahili nukuu hiyo ya juu inasomeka: “Petro mbarikiwa anaonekana kuwa amefanyika KASISI WA MWANA WA MUNGU duniani.”
,
Nukuu mbili za kilatini zifuatazo zote zina maana ileile kama ya moja hapo juu, na zote zinatumia jina la Vicarius Filii Dei,, Ya kwanza inasema:
_
“Beatus Petrus in terris VICARIUS FILII DEI esse videtur constitutus.” —(Corpus Juris Canonici, Gregorii XIII, Pontif. Max., Auctoritate, Distinctio 96, Column 286, Canon Constantinus 14, Magdeburg, 1747.
Jina alilopewa Papa ni “Vicarius Filii Dei.” Sacrosancta concilia ad regitionem exacta, na Philippe Labbe, SJ., Vol. I, p 1534: Paris, 1671).
,
Nukuu hiyo hiyo tena, lakini inatoka kwenye kitabu kingine tofauti inasema:
,
“Beatus Petrus in terris VICARIUS FILII DEI esse videtur constitutus.” —(Corpus Juris Canonici Emendatum et Notis Illustratum Gregorii XIII. Pont. Max., Lvgdvn., MDCXXII, col. 295).
,
Ni mkatoliki pekee ambaye aidha ana kichwa kigumu au moyo mgumu ndiye atakataa ushahidi wote huu, na kupinga kwamba VICARIUS FILII DEI--666--sio jina la papa. Ukweli ni kwamba kuna maelfu ya dokomenti za katoliki zinazokili kwamba Vicarius Filii Dei ni jina la papa! Lakini hatutaki kukuchosha kwa kusoma maneno mengi. Tunaamini kwa haya machache utachukua hatua ya kuchunguza na kuhakikisha wewe mwenyewe. Na tunaomba ufanye hivyo kwa Jina la Yesu Kristo.