Jumanne, 11 Julai 2017

WALIMU WA KANISA

Mwalimu wa kanisa ni jina la Heshima Ambalo kwa Nadra kanisa Katoliki linampa Mtakatifu, Ambaye ktk maisha ,Mafundisho na Maandishi yake alionesha Na Kueneza Mwanga wa pekee ktk Masuala ya Imani ,Maadili na Maisha ya kiroho.

     Tamko la Kwamba Mtakatifu Fulani ni Mwalimu wa kanisa lote linategemea Utambuzi wa Karama maalum ya hakima Ambayo alijaliwa na Roho Mtakatifu kwa Faida ya kanisa ikibainishwa  na athari njema ya Mafundisho yake ktk Taifa la Mungu.(Papa Benedicto XVI, Barua ya kitume ya 7 October 2012).

Mpaka sasa,ktk miaka karibu 2000 ni Mababu wa kanisa wanne muhimu zaidi upande wa magharibi :

•Gregori (540-640)-1298*
•Ambrosi wa mirano(340-397)-1298*
•Augustino wa Hippo,Doctor Gratiae (354-430)-1298*
•Jerome (347-420)-1298*

Mwaka 1568 Walitangazwa mababu wa kanisa wanne muhimu zaidi upande wa Mashariki, pamoja na Thoma wa Akwino ,Mwalimu bora wa karne za kati Upande wa Magharibi.

•Yohane Krisostomo(347-407)-1568*
•Basili (329-379)-1568*
•Gregori wa Nazianzo(329-390)-1568*
•Thoma wa Akwino,Doctor Angelus (1225-1274)-1568*

Na Baadaye waliendelea kutangazwa kama ifuatavyo:

•Bonaventura wa Bagnoregio, Doctor Seraphicus (1217-1274)-1588

•Anselm wa Canterbury, Doctor Magnificut (1033-1109)-1720
•Isidori wa sevilla (560-636)-1722*
•Petro Krisologo(450-580)-1729*
•Leo I (400-461)-1754*
•Petro Damian(1007-1072)-1828
•Bernardo wa Claivaux,Doctor Mellifluous (1090-1153)-1830
•Hilari wa Poitiers (315-367)-1851
•Alfonso Maria wa Liguori,Doctor Zelantissimus(1696-1787)-1871
•Francisco wa sales (1567-1622) Doctor caritatis 1877
•Sirili wa Alexanderia,Doctor Incarnationis (370-444)-1883*
•Sirili wa Yerusalem* (315-386)-1883
•Yohane wa Damasco (676-749)-1883
•Beda (672-735)-1899*
•Efrem Mshamu (306-373)-1920*
•Petro Kanisi (1521-1597)-1925
•Yohane wa Msalaba, Doctor Mysticus (1542-1591)-1926
•Roberto Bellarmino (1542-1621)-1931
•Alberto, Doctor Universalis (1205-1280)-1931
•Antoni wa Padua Doctor Evangelicus (1195-1231)-1946
•Laurenti wa Brindisi, Doctor Apostolicus (1559-1619)-1959
•Teresa wa Yesu {1515-1582)-1970
•Katerina wa Siena (1347-1380)-1970
•Theresa wa Mtoto Yesu Doctrix Amoris (1873-1897)-1997
•Hildegarda wa Bingen (1098-1179)-2012
•Yohane wa Avila (1500-1569)-2012

      Mwaka wa kutangazwa ukifuatwa na Nyota unaonesha Wanaoheshimiwa na Waorthodoksi pia, ingawa kwao Hakuna Cheo cha Mwalimu wa Kanisa .

       Tofauti na orodha hiyo hapa chini tutawapitia Mmoja Mmoja kufuatana na Historia ya Kanisa ,kuanzia mababu wake wa Karne IV Hadi Mwalimu wa Mwisho aliyefariki mwaka 1897 tu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni